Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, katika picha ya pamoja na menejimenti za Taasisi za Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) katika kikao kazi cha uwasilishwaji wa taarifa za majukumu ya Taasisi hizo kilichofanyika jijini Dodoma Septemba 26, 2023.
Sehemu ya Menejimenti za Taasisi za Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majego na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa (hayupo pichani), katika kikao kazi cha uwasilishwaji wa taarifa za majukumu ya Taasisi hizo kilichofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent L. Bashungwa, akizungumza na menejimenti za Taasisi za Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) katika kikao kazi cha uwasilishwaji wa taarifa za majukumu ya Taasisi hizo kilichofanyika jijini Dodoma Septemba 26, 2023. Katika kikao hicho Waziri Bashungwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Eng. Aisha Amour na sehemu ya Menejimenti ya Wizara.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akiteta jambo na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel, katika mkutano wa hadhara wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na wananchi uliofanyika katika Uwanja wa Mitwero mkoani Lindi tarehe 19 Septemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa na viongozi wengi akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Nachingwea – Ruangwa, sehemu ya Ruangwa – Nanganga (km 53.2) inayojengwa kwa kiwango cha lami, leo tarehe 18 Septemba 2023
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Nachingwea – Ruangwa, sehemu ya Ruangwa – Nanganga (km 53.2) inayojengwa kwa kiwango cha lami, leo tarehe 18 Septemba 2023.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa na viongozi wengine wakati akiwasili katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Nachingwea – Ruangwa, sehemu ya Ruangwa – Nanganga (km 53.2) inayojengwa kwa kiwango cha lami, leo tarehe 18 Septemba 2023. Mgeni Rasmi katika hafla hiyo ni Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Eng. Aisha Amour, akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Frank Chonya, mara walipotembelea Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Majaliwa uliopo Wilayani humo mkoani Lindi, Septemba 17, 2023. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Mohamed Besta.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Eng. Aisha Amour pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Eng. Mohamed Besta, wakati wakikagua maandalizi ya sherehe ya uwekaji jiwe la Msingi wa barabara ya Ruangwa - Nanganga (km 53 5), utakaofanyika Septemba 18, 2023 katika kijiji cha Nandagala mkoani Lindi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Eng. Aisha Amour akitoa maelekezo wakati akikagua maandalizi ya uwekaji jiwe la msingi wa barabara ya Ruangwa - Nanganga (km 53 5), utakaofanyika Septemba 18, 2023 katika kijiji cha Nandagala mkoani Lindi.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa (katikati), akisikiliza kwa makini hoja za wananchi wakati wa Ziara ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Mtwara ikiwa ni siku ya pili katika mkoa huo ambapo amekagua miradi mbalimbali na kuzungumza na wananchi katika Halmashauri ya Nanyamba pamoja na Newala.
Naibu Waziri Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya (kushoto), akiwa Kwenye mkutano wa nne wa Mawaziri wa Masuala ya Uchukuzi, Miundombinu na Nishati wa Bara la Afrika uliofanyika kuanzia tarehe 12 -15 SEPTEMBA, 2023 Zanzibar ambapo nchi 41 kati ya 55 zimeshiriki katika mkutano huo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi (hawapo pichani), waliofika kushuhudia uwekaji wa Jiwe la msingi la Ufunguzi wa Barabara ya Mtwara - Newala - Masasi, sehemu ya Mtwara - Mnivata yenye urefu wa kilometa 50 iliyogharamiwa na Serikali kwa 100% kwa gharama ya jumla ya Shilingi Bilioni 93.83, tarehe 14 Septemba 2023, mkoani Mtwara,
Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa, akizungumza na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, mkoani Mtwara.
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa, akisalimia katika mkutano wa hadhara na wananchi uliofanyika katika Uwanja wa Majaliwa Wilayani Tandahimba, mkoani Mtwara, Septemba 16, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa pamoja na Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa wakati alipowasili Uwanja wa Ndege wa Mtwara kupokea taarifa ya uendelezaji wa Kiwanja hicho (ukarabati na upanuzi) ambao umefikia asilimia 98% chini ya usimamizi wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), tarehe 15 Septemba 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta wakati akipokea taarifa ya uendelezaji wa Kiwanja cha Ndege cha Mtwara ambacho kimefikia asilimia 98 chini ya usimamizi wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) tarehe 15 Septemba 2023.
Muonekano wa Barabara ya Mtwara - Newala- Masasi, sehemu ya Mtwara - Mnivata (Km 50) ambayo imefunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan leo tarehe 15 Septemba 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa pamoja na viongozi wengine akikata utepe kuzindua barabara ya Mtwara - Newala- Masasi, sehemu ya Mtwara - Mnivata (Km 50) leo tarehe 15 Septemba 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan akiweka jiwe la msingi la ufunguzi wa barabara ya Mtwara- Newala-Masasi, sehemu ya Mtwara-Mnivata (Km 50) iliyogharamiwa na Serikali kwa asilimia 100 kwa gharama ya shilingi Bilioni 93.83 leo tarehe 15 Septemba 2023. Kushoto ni Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya akizungumza na wahandisi wakati wa Mkutano wa 20 wa Wahandisi uliofanyika Mlimani City, Dar es Salaam jana.
Wahandisi wataalamu wapya wakila kiapo mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati wa Mkutano wa 20 wa Wahandisi uliofanyika Mlimani City, Dar es Salaam jana
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali, Ahmed Abbas mara baada ya kuwasili mkoani humo ikiwa ni maandalizi ya ziara ya kikazi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani humo inayoanza leo tareh 14 -17/09/2023
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta wakati alipofanya ziara Makao Makuu ya TANROADS ikiwa ni ziara ya ya kwanza kwenye taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi, leo tarehe 12 Septemba 2013.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa (katikati) akifurahia jambo na Mbunge wa Iramba ambaye pia ni Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba wakati wa Hafla ya Kumkabidhi Mkandarasi Henan Highway Engineering Group kujenga barabara ya Sabasaba-Sepuka-Ndago-Kizaga (KM 77.6) mkoani Singida.