Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akifunua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Daraja la J.P Magufuli (Km 3) mkoani Mwanza Juni 19, 2025.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli akisaini kitabu cha Wageni alipotembelea banda la Wizara ya Ujenzi katika maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 19, 2025 Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Banda la Wizara ya Ujenzi Juni 18, 2025 katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025, Chinangali Park jijini Dodoma.
Watumishi wa Wizara ya Ujenzi wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara hiyo katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. Maonesho hayo yanaongozwa na kaulimbiu "Himiza matumizi ya mifumo ya kidijitali ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji".
Wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi, Wakala ya Barabara (TANROADS) na wapandaji miti kutoka Jeshi la Kujenga Taifa -Makutupora wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukamilisha zoezi la upandaji miti 150 pembezoni mwa barabara ya mzunguko wa nje wa jiji la Dodoma kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani 2025.
Wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi, Wakala ya Barabara (TANROADS) na wapandaji miti kutoka Jeshi la Kujenga Taifa -Makutupora wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukamilisha zoezi la upandaji miti 150 pembezoni mwa barabara ya mzunguko wa nje wa jiji la Dodoma kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani 2025.
Mhandisi Mkuu, Chacha Harun kutoka Kitengo cha Usalama na Mazingira, Wizara ya Ujenzi akitoa elimu kwa sehemu ya Menejimenti ya Wizara hiyo ilipotembelea na kukagua banda la Wizara ya Ujenzi na Wakala ya barabara (TANROADS), leo Juni 3, 2025 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre, jijini Dodoma yanapofanyika maonesho ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani 2025.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi, Godfrey Kasekenya akimpa zawadi Makamu wa Waziri wa Ardhi, Miundombinu na Usafirishaji wa Jamhuri ya Korea, Mhe. Hyun Hwan Jin mara baada ya kumaliza kikao chao kilichofanyika katika Ofisi za Wizara hiyo jijini Dodoma leo, Mei 27, 2025
Muonekano wa sehemu ya barabara ya mzunguko wa nje ya Dodoma (Dodoma Outer Ring Road) ambayo kwa sasa utekelezaji wake umefika zaidi ya asilimia 85.
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, kutoka Wizara ya Ujenzi, Bw. Mrisho Mrisho (katikati mbele) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi hodari pamoja na wawakilishi wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo mara baada ya kugawa zawadi ya vyeti na fedha taslimu kwa watumishi Hodari wa Idara na Vitengo kwa mwaka wa Fedha 2024/2025 leo, Mei 20,2025 jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amepokea Taarifa ya Kamati ya uchunguzi ya Kivuko cha MV. Tanga kinachotoa huduma wilayani Pangani, Mkoani Tanga leo Mei 20, 2025 Ofisini kwake jijini Dodoma. Kamati hiyo aliiunda Mei 13, 2025 alipofanya ziara mkoani Tanga na kuipa siku Saba kuchunguza changamoto zinazojitokeza mara kwa mara katika kivuko hicho baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kuhusu kusuasua kwa utendaji wake.
Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala leo, tarehe 20 Mei, 2025 Ofisini kwake, jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma leo, Mei 05, 2025 wakati wa uwasilishaji wa hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Balozi, Mhandisi Aisha Amour akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma leo, Mei 05, 2025 wakati wa uwasilishaji wa hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi, Godfrey Kasekenya (kulia) akimpongeza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega mara baada ya kuwasilisha Bungeni Mpango na makadirio ya Mapato na Matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2025/2026 leo tarehe 05 Mei, 2025 mkoani Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega akiwasilisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2025/ 2026, Bungeni jijini Dodoma leo Mei 05, 2025. Waziri huyo ameomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi Trilioni 2.28 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega akiwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Godfrey Kasekenya wakiwasili Bungeni jijini Dodoma leo tarehe 05 Mei, 2025 kushiriki vikao vya Bunge la Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ambapo leo Waziri huyo amewasilisha Mpango na makadirio ya Mapato na Matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima wakikagua athari za mvua katika miundombinu ya barabara ya Ifakara - Malinyi yaliyosababisha kukatika kwa mawasiliano ya barabara hiyo Mkoani Morogoro.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa na Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega leo Aprili 16, 2025 akikagua eneo la Matandu na Somanga Mtama barabara kuu ya Dar es Salaam - Lindi yaliyokuwa yamekatika hivi karibuni kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Wilayani Kilwa Mkoani Lindi.
Magari yakiendelea kuruhusiwa kupita katika eneo la Somanga Mtama Mkoani Lindi tarehe 10 Aprili, 2025 mara baada ya eneo hilo kukarabatiwa na kuimarishwa huku ujenzi wa daraja la kudumu ukiendelea.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega akisalimiana na Dereva wa lori wakati alipokuwa akikagua hali ya Miundombinu ya barababara ilivyoimarishwa katika eneo la Somanga Mtama na Matandu Mkoani Lindi, tarehe 10 Aprili, 2025.
International Conference on Transport Asset Management 2025
International Conference on Transport Asset Management 2025
Muonekano wa daraja la J.P Magufuli (Kigongo Busisi) KM 3, mkoani Mwanza. Daraja hili limegharimu zaidi ya Shilingi bilioni 610 na limefikia asilimia 97 kwa sasa.
Muonekano wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka, Dar es Salaam Awamu ya Nne (BRT 4) kuanzia Ubungo Daraja la Kijazi (Sam Nujoma) - Mwenge - Maktaba ya Taifa (Posta) yenye urefu wa kilometa 13.5.